Apple yaongeza bei ya laptopu na kompyuta zake

23:00






Kampuni ya teknolojia ya Apple imeongeza bei ya laptopu na kompyuta zake nchini Uingereza kwa pauni 100.
Siku ya Alhamisi ,kampuni hiyo ilizindua laptopu za Macbook Pro zikiwa na bei sawa na ile ya Marekani.
Lakini kampuni hiyo pia iliongeza bei ya tarakilishi zake ,ikiwemo ile ya Mac Pro ilio na miaka mitatu kwa pauni 100.
Mchanganuzi mmoja alisema kuwa wateja wanafaa kutarajia kuongezwa kwa bei hizo zaidi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »