Saa
cahche baada ya kuvishwa taji, kumeibuka upotoshaji mkubwa kutoka kwa
baadhi ya watu wenye nia ovu ya kutaka kuharibu taswira nzima ya Mshindi
wa shindano la Miss Tanzania 2016, aliyevishwa taji hilo jana usiku
ndani ya jiji la Mwanza,taarifa hizo ambazo zimekuwa zikisambazwa katika
mitandao ya kijamii zikieleza upotoshaji wa taarifa mbalimbali za
mlimbwende huyo zikiwemo na elimu yake.
SEHEMU YA TAARIFA ILIYOKUWA IKIPOTOSHWA KATIKA MITANDAO MBALIMBALI YA KIJAMII HII HAPA CHINI;
MISS TANZANIA 2016
JINA:Diana Edward Lukumai
UMRI:Miaka 18
ELIMU:Shahada(degree)
Hii ina maana;
Alianza Chuo akiwa na miaka 15
Alianza Form one akiwa na miaka 9
Ingawa
sio mshabik wa haya mambo napenda nchukue hii nafasi kuwapongeza Wazazi
wote kama wazazi wa Diana ambao watoto wao wameanza shule ya msingi
wakiwa na miaka miwili
HII NDIO TAARIFA SAHIHI YA MSHINDI WA SHINDANO LA MISS TANZANIA 2016,DIANA EDWARD LOY.
Napenda kuujulisha Umma yafuatayo;
1.
Miss Tanzania 2016/2017 aliyeshinda taji jana jijini Mwanza, anaitwa
Diana Edward Loy na siyo Diana Lukumai kama inavyotajwa mitandaoni.
2.
Mlimbwende huyo amemaliza kidato cha nne 2015 Shule ya Sekondari Arusha
Day na si 2011 kama inavyotajwa mitandaoni kwa malengo ovu.
3.
Diana hajawahi kujiunga na Elimu ya Chuo Kikuu chochote Tanzania au
duniani bali anatarajia kujiunga mwaka huu katika chuo cha IFM kusomea
masula ya kodi ngazi ya stashahada (cheti) ingawa kulingana na ratiba
zake na majukumu yake mapya ikiwemo kushiriki Miss world mapya huenda
akaahirisha mwaka wake wa masomo.
4.
Tunawasihi watanzania kutumia vyema mitandao ya kijamii na si kufanya
"Character assassination" lakini pia tunaheshimu haki yao ya msingi ya
kuhoji masuala ya msingi kabisa kuhusu mtu ambaye ni Public figure na
ataliwakilisha taifa katika anga za kimataifa.
EmoticonEmoticon