Jamaa akiri kujaribu kuingia ndani ya nyumba ya Rooney

11:43

Mwanamume mmoja amekiri kujaribu kuingia ndani ya nyumba ya Wayne Rooney wakati mchezaji soka huyo alipokuwa katika mechi uwanjani Old Trafford.

Mwanajeshi wa zamani, Robert McNamara, mwenye umri wa miaka 24, kutoka Scarborough, amekiri makosa katika mahakama ya Chester Crown kwa kujaribu kuingia katika nyumba hiyo pasi idhini akiwa na nia ya kuiba.

Mnamo Agosti 3 King'ora kililia katika nyumba hiyo yenye thamani ya pauni milioni 6 huko Prestbury, Cheshire.

McNamara atahukumiwa Desemba 21.

Jaji Nicholas Woodward amesema kulikuwa na mambo ya kutia wasiwasi katika kesi hiyo na kuagiza kitengo cha dhamana mahakamani kukusanya ripoti ya kabla hukumu kutolewa.

Rooney, mkewe Coleen, na watoto wao watatu, Kai, Klay na Kit, walikuwa wamehudhuria mechi ya kuchangisha fedha za misaada dhidi ya timu alioichezea kwanza Rooney, Everton, wakati jaribio hilo la wizi lilipotokea.

McNamara alikamtwa siku sita baadaye.

Upande wa mashtaka haukueleza upande wake wa kesi hiyo lakini mahakama ilielezewa kuwa hivi karibuni McNamara amegunduliwa kuugua matatizo ya akili na kuwa familia yake ilitafuta usaidizi kutoka taasisi inayotoa huduma ya afya kwa magonjwa ya akili, mapema mwaka huu.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »