News: Bondia Thomas Mashali auwawa, mwili wake waokotwa vichakani Dar

23:06
Bondia maarufu wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali, hatunaye.Taarifa zinaeleza ameuwawa kwa kupigwa risasi na mwili wake kuokotwa vichakani maeneo ya Kimara jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo.

Yassin Abdallah maarufu kama Ustaadhi, mmoja wa viongozi wakongwe wa mchezo wa ngumi amethibitisha na kusema mwili wa Mashali upo kwenye chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
"Tumethibitishiwa hizo taarifa za majonzi kabisa, mwili upo Muhimbili na msiba upo kwao Tandale," alisema Ustaadhi.
 



 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »