Bila shaka
umeshawahi kufikiria kuhusu mrithi wa mali zako siku ikitokea haupo
duniani, japokuwa kwa tamaduni za kiafrika ni watu wachache sana huwa
wanaweka wazi au kuandika taarifa kuhusu warithi wa mali zao pindi
ikitokea wamefariki dunia.
Sasa leo nimeipata hii kuhusu atakayerithi mali au utajiri wa Bill Gates ambaye ni tajiri namba moja wa dunia kwasasa.
Kwa mujibu
wake mwenyewe Gates amesema hataacha utajiri wake unaotajwa kufikia
Dola za Marekani Bilioni 81.7 kwa watoto wake watatu na badala yake
atatoa kiasi dola za Marekani Bilioni 70 kwa watu wanaohitaji msaada
dunia nzima, na tayari watoto wake wote wanajua kuhusu maamuzi yake na
wamemuelewa.
Akizungumza
kupitia kipindi cha Holly Willoughby na mtangazaji Ben Shephard,
Mmiliki huyo wa kampuni ya Microsoft mwenye miaka 60 amesema “Ndio,
watoto wetu wanapata elimu bora sana na tunawapa pesa za kutosha lakini
kuna siku watakwenda kuanza maisha yao na kufanya kazi zao.” – Bill
Gates
Bill Gates
amesema kuwa endapo ataruhusu watoto wake wawili wakike na mmoja wa wa
kiume warithi utajiri wake watakachokifanya ni kuzichezea tu pesa zake.
Mfanyabiashara
huyo mkubwa amesema kuwa ana uhakika watoto wake hawawezi kuwa masikini
na ameshawawekea uhakika wa maisha yao watakapoanza maisha yao siku za
baadaye. Bill Gates na mkewe Mellinda mwenye miaka 52 wana watoto watatu
ambao Jennifer mwenye miaka 20, Rory mwenye miaka 17, ana Phoebe mwenye
miaka 14.
EmoticonEmoticon